Isaya 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20023 majemadari na wakubwa, washauri, wachawi wafundi na waganga wenye maarifa. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Hivyo nikatwaa wale viongozi wenye hekima, akili na ujuzi ambao muliwachagua kutoka katika makabila yenu, nikawaweka kuwa viongozi wenu. Nikawaweka wengine kuwa majemadari wa makundi ya watu elfu moja moja, ya watu mia moja moja, ya watu makumi tano tano na ya watu kumi kumi. Nikachagua vilevile wakubwa wengine wa kuchunga kila kabila.
Atajichagulia wengine wakuwe wakubwa wa makundi ya waaskari wake wa maelfu na wengine wakuwe wakubwa wa makundi ya watu makumi tano. Atawafanya wengine wamulimie mashamba yake na kuvuna mazao yake. Atawafanya wengine vilevile wamutengenezee silaha za vita, na wengine wamutengenezee vyombo vya magari yake.