Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 3:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Halafu watu watalia na kuomboleza kwenye milango ya muji; nao wataikaa ndani ya mavumbi katika ukiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 3:26
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wakaikaa kwenye udongo pamoja na Yobu kwa siku saba, muchana na usiku, bila kumwambia neno lolote maana waliona mateso yake kuwa makubwa sana.


Yobu akatwaa kigae, akajikuna nacho na kuikaa kwenye majivu.


Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Maana nyumba ya kifalme itaachwa ukiwa, muji huo wa watu wengi utahamwa. Mulima na munara wa ulinzi utakuwa mapango milele, punda wa mwitu watapitapita huko kwa furaha, kondoo watapata malisho yao humo.


Inchi inaomboleza na kunyauka; pori ya Lebanoni imekauka, bonde zuri la Saroni limekuwa jangwa, kule Basani na mulima Karmeli majani yote yamekauka.


Shuka, uikae katika mavumbi, ewe bikira, binti wa Babeli! Ikaa chini pasipo kiti cha kifalme, ewe binti wa Wakaldea! Tokea sasa hautaitwa tena murembo wala mwenye kupendeza.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Watu wa Yuda wanaomboleza, miji yake inateketea. Watu wake wanaomboleza wakiikaa katika udongo na kilio cha Yerusalema kinapanda mpaka juu.


Wajane wao wamekuwa wengi kuliko muchanga wa bahari. Nao wamama wenye watoto vijana nimewaletea mwangamizaji muchana kati. Nimesababisha uchungu na vitisho viwapate kwa rafla.


Namna gani muji uliokuwa umejaa watu, sasa unakaa peke yake! Ulikuwa na utukufu kati ya mataifa, sasa umekuwa kama mama mujane. Ulikuwa kama binti wa mufalme kati ya miji, sasa umekuwa mutumwa.


Barabara za Sayuni zinaomboleza, maana hakuna anayepita kwa sikukuu. Milango yake yote ni tupu, makuhani wake wanaugua, wabinti zake wana huzuni, na muji wenyewe uko katika uchungu.


Wazee wa Sayuni wameikaa chini kimya, wamejitia mavumbi juu ya vichwa na kuvaa gunia. Wabinti wa Yerusalema wameinamisha vichwa chini.


Yawe alikusudia kuubomoa ukuta wa Sayuni; aliupima na kuhakikisha kila kitu kwamba kimeharibika; minara na kuta za inje ya muji akazifanya ukiwa, zote kwa pamoja zikaangamia.


Miji yenye watu itateketezwa, na inchi itakuwa ukiwa. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Wakubwa wote wa mataifa ya kandokando ya bahari watashuka toka kwenye viti vyao vya kifalme, na kuvua nguo zao za heshima pamoja na nguo zao zilizopindwa. Kisha kujaa hofu, wataikaa chini; nao watatetemeka wakati wote na kushangaa sana juu ya hayo yaliyokupata.


Vidonda vya Samaria haviwezi kupona, navyo vimeipata vilevile inchi ya Yuda; vimefikia kwenye mulango wa Yerusalema, pahali watu wangu wanapokaa.


‘Tuliwapigia ngoma, lakini hamukucheza! Tuliimba wimbo wa kilio, lakini hamukulia!’


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ