Peka, mwana wa Remalia akawaua watu wengi sana. Aliua waaskari mashujaa wa Yuda elfu mia moja na makumi mbili katika siku moja. Ilitokea vile kwa sababu walimwacha Yawe, Mungu wa babu zao.
Nikienda inje katika mbuga, ninaiona maiti ya waliouawa kwa vita; nikiingia ndani katika muji, ninaona tu maiti ya waliokufa kwa njaa! Manabii na makuhani wanashugulikia mambo yao katika inchi, lakini hawajui wanalofanya.
Wajane wao wamekuwa wengi kuliko muchanga wa bahari. Nao wamama wenye watoto vijana nimewaletea mwangamizaji muchana kati. Nimesababisha uchungu na vitisho viwapate kwa rafla.
Kwa hiyo uwaache watoto wao wakufe kwa njaa, uwaache wakufe kwa vita. Wake zao wakuwe tasa na wajane. Waume zao wakufe kwa magonjwa makali na vijana wao wachinjwe kwa upanga katika vita.
Vilevile kwa nafasi hii nitaivuruga mipango ya watu wa Yuda na ya watu wa Yerusalema. Nitawatoa washindwe na kuuawa kwa panga na waadui zao, wale wanaovizia maisha yao. Nazo maiti zao nitaziacha kuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.
Mutu atakayebaki katika muji huu atauawa kwa vita au kwa njaa au kwa magonjwa makali. Lakini mutu atakayetoka inje ya muji huu na kujitoa kwa Wababeli wanaozunguka ukuta wake, ataishi; kweli ataokoa maisha yake.
Maiti za vijana na wazee zimelala ndani ya mavumbi katika barabara, wabinti na vijana wangu wameuawa kwa upanga; umewaua bila huruma siku ya hasira yako.