Halafu nilimwuliza: ‘Wewe ni binti ya nani?’ Akaniambia: ‘Mimi ni binti ya Betueli mwana wa Milka, muke wa Nahori.’ Halafu nikamupa pete na kumuvalisha vikomo kwa mikono.
Halafu, mufalme akavua pete yake ya muhuri kwenye kidole chake na kumuvalisha Yosefu. Akamuvalisha na nguo za kitani safi na mukufu wa zahabu kwa shingo.
Hivyo wote wenye moyo safi, wanaume na wanawake, wakaleta pete za masikio na za muhuri, vikuku na kila aina ya mapambo ya zahabu. Kila mutu akamutolea Yawe kitu cha zahabu.
Mikono yake ni kama pete za zahabu, amevaa mawe ya bei kali. Kiwiliwili chake ni kama pembe za tembo zilizopambwa kwa mawe ya yakuti ya rangi ya samawi.
Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: ‘Mulete mbio kanzu nzuri sana na kumuvalisha nayo. Mumuvalishe pete kwenye kidole chake na mumuvalishe viatu.
Kwa mufano: tajiri mumoja anayevaa pete ya zahabu na nguo nzuri anaingia katika nyumba yenu ya kuabudia. Na kisha kunaingia vilevile masikini anayevaa nguo zinazopasukapasuka.