Hapo Sadaka na Kivuli wakasema: “Utuue wewe mwenyewe, maana hii ni kazi ya mutu muzima.” Gideoni akawaua yeye mwenyewe na kutwaa mapambo yao yaliyokuwa kwenye shingo la ngamia wao.
Uzito wa pete zote alizoomba wamupe ulikuwa kilo makumi mbili. Zaidi ya hivyo, alipokea vilevile vyuma vya masikio, nguo za rangi nyekundu-nyeusi zilizovaliwa na wafalme wa Midiani na mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia wao.