Wakubwa wa Wamisri wakawapiga wasimamizi wa Waisraeli waliochaguliwa kusimamia kazi wakisema: “Kwa nini hamutimizi kazi yenu na kufikisha hesabu ileile ya matofali kama mbele?”
Wazaliwa wa kwanza wa wazaifu watashiba, na wakosefu watakaa kwa usalama. Lakini chipukizi wenu nitawaua kwa njaa; na yeyote kati yenu atakayebaki nitamwua.
Wapumbafu wanasema maneno ya upumbafu, na mafikiri yao ni kutenda maovu, kutenda mambo ya watu wasiomujua Mungu, kusema maneno ya kumutukana Yawe. Wanawaacha wenye njaa bila chakula, na wenye kiu wanawanyima kinywaji.
Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!
Kwa nini munarudiliarudilia mezali hii katika inchi ya Waisraeli: Wababa wamekula matunda mabichi ya mizabibu, lakini ni meno ya watoto wao ndiyo yanaumizwa!
Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.