13 Yawe yuko tayari kuanza mashitaki, anasimama kwa kuwahukumu watu wake.
Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”
Ee Mungu, simama sasa ujitetee! Ukumbuke mazarau ya kila siku ya wasiokujua.
Zaburi ya Asafu. Mungu anasimamia baraza lake. Anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:
Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.
Bwana, Yawe, Mungu wako, anayewatetea watu wake, anasema hivi: Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha, hautakunywa tena kikombe cha kasirani yangu.
Yawe atatoa hukumu kwa moto atawaazibu watu wote kwa upanga; nao atakaowaangamiza watakuwa wengi.
Musikilize jinsi Yawe anavyosema: Wewe nabii, kwenda ukailalamikie milima, navyo vilima visikie sauti yako.
Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.