Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”
Wenye zambi wanatenda maovu mara mia. Hata hivyo, wanaendelea kuishi. Lakini, mimi ninajua kwamba itakuwa heri kwa wanaomwogopa Mungu, kwa sababu ya woga wao.
Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.
Basi, ee Yawe, acha laana hizo zinipate kama sikukutumikia vizuri na kama sikukusihi kwa ajili ya waadui zangu wakati walipokuwa katika taabu na shida!
Unazani umekuwa mufalme kwa kujenga na mierezi? Baba yako alikula na kunywa, alifuata sheria yangu na kutenda mambo ya haki, na mambo yake yaliendeka vizuri.
Lakini niliwapa amri kwamba waitii sauti yangu kusudi nikuwe Mungu wao, nao wakuwe watu wangu. Niliwaamuru vilevile waishi kama nilivyowaagiza, kusudi wapate uheri.
Atakayetenda zambi huyo ndiye atakayekufa. Mutoto hatabeba uovu wa baba yake, wala baba hatabeba uovu wa mutoto wake. Uhaki wa mutu wa haki itamufalia yeye mwenyewe: na uovu wa mwovu ataubeba yeye mwenyewe.
akamwambia hivi: Pita katikati ya Yerusalema, upate kutia kitambulisho kwenye vipaji vya nyuso za watu wanaohuzunika na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika muji huu.
Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.
Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.