Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa, Bwana wetu Yawe wa majeshi ataondoa kutoka Yerusalema na inchi ya Yuda kila tegemeo: tegemeo lote la chakula na la kinywaji.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 3:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika siku ya tisa ya mwezi wa ine njaa ilikuwa kali sana katika muji hata hakukuwa chakula chochote kwa ajili ya wakaaji wake.


Mungu alileta njaa katika inchi yao, akafunga njia zao zote za kupata chakula.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?


Yawe anasema: Wanawake wa Sayuni wako na kiburi; wanatembea wakiinua kichwa juu, wakirembua macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, nao wanalilisha mikufu kwenye miguu yao.


Yule jemadari akawaambia: “Munazani kwamba bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Maneno yangu ni vilevile kwa watu wanaoikaa juu ya ukuta! Bado kidogo wao kama vile ninyi watakula mavi yao wenyewe na kunywa mikojo yao wenyewe!”


Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho kwa sababu ya ukosefu wao wa akili. Wakubwa wao watakufa na njaa, watu wengi watakufa na kiu.


Bwana, Yawe, Mungu wako, anayewatetea watu wake, anasema hivi: Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha, hautakunywa tena kikombe cha kasirani yangu.


Manase anashambulia Efuraimu, Efuraimu anashambulia Manase na wote wawili wanashambulia Yuda. Hata hivyo, hasira ya Yawe haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Basi, mufalme Zedekia akatoa amri Yeremia awekwe katika chumba cha walinzi na kupewa mukate kila siku kutoka kwa wapikaji wa mukate mpaka mikate ilipotoweka kabisa huko katika muji. Basi, Yeremia alibaki katika chumba cha walinzi.


Bwana wangu mufalme, watu hawa wamefanya kitu kibaya. Wamemutia yule nabii Yeremia katika kisima ambamo kwa kweli atakufa kwa njaa, kwa maana hakuna chakula tena katika muji.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Katika siku ya kenda ya mwezi wa ine, njaa ilikuwa kali sana katika muji hata hakukukuwa chakula chochote kwa ajili ya wakaaji wake.


Maji yetu tunayapata kwa feza, kuni zetu kwa kuzinunua.


Wewe mwanadamu! Taifa fulani likitenda zambi kwa kukosa uaminifu kwangu, mimi nitanyoosha mukono wangu kwa kuliazibu. Nitaiharibu akiba yake ya chakula na kuliletea njaa. Nitawaua watu na nyama wake.


Chakula chenu nitakipunguza hata wanawake kumi watumie mafika moja tu kwa kupika mikate. Watawagawanyia mukate wenu kwa kipimo. Na hata kisha kula mutaendelea kuwa na njaa tu.


Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Sasa kwa nini munalia kwa sauti? Hamuna mufalme tena? Mushauri wenu ametoweka? Munalalamika kwa uchungu, kama mwanamuke anayezaa!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ