Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.
Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!
Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.
Nawe utawajibia hivi: Yawe anasema hivi: Nitawalewesha wakaaji wote wa inchi hii; wafalme wanaotawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi, makuhani, manabii na wakaaji wote wa Yerusalema.
Ujumbe juu ya manabii wasiofaa. Nimevunjika moyo, mifupa yangu yote inatetemeka; nimekuwa kama mulevi, kama mutu anayetabanika na pombe, kwa sababu ya Yawe na maneno yake matakatifu.
Yawe akaniamuru: Utawaambia kwamba: Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Mukunywe, mulewe na kutapika; muanguke wala musisimame tena, kwa sababu ya mauaji nitakayosababisha kati yenu.
Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi, mushangilie na kufurahi kwa sasa. Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile. Mutakikunywa na kulewa, hata mutavaa uchi!
Kisha akarudi kwenye wanafunzi wake na kuwaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Angalia, saa imetimia, sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.
Aliporudi kwa mara ya tatu, akawaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Inatosha! Saa imetimia. Sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.
Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.