Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 29:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema yatakuwa kama mutu mwenye njaa anayeota ndoto kwamba anakula lakini anaamuka angali bado na njaa, na kama mutu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa lakini anaamuka muzaifu, na angali bado na kiu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 29:8
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Wafezeheke na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia Sayuni.


Ee Bwana, unapoinuka, wanatoweka kama ndoto, kama ndoto wakati mutu anapoamuka.


Kweli! Wote waliokukasirikia, watapata haya na kufezeheka. Wote wanaopingana nawe, watakuwa wa bure na kuangamia.


Utawatafuta hao wanaopingana nawe, hautawaona tena; wale wanaofanya vita nawe, watakuwa wameangamia.


Mufuaji wa vyuma anatwaa kipande cha chuma, anakiyeyusha kwa moto na kufua sanamu. Anakipondaponda na nyundo kusudi akipatie umbo kwa mikono yake yenye nguvu. Wakati wote huo yeye anasikia njaa na kuchoka; anasikia kiu na nguvu kuregea.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Enyi watu wa Yuda muangalie: Mutu anakuja kutoka milima anayeleta habari njema, anayetangaza amani. Mufanye sikukuu zenu, mutimize viapo vyenu, maana waovu hawatawashambulia, kwa sababu wameangamizwa kabisa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ