Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 29:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 29:5
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, wapeperushwe kama majani yenye kukauka, wakuwe kama maganda yanayopelekwa na zoruba!


Lakini waovu si vile hata kidogo. Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.


Wakuwe kama maganda yanayopeperushwa na upepo, wakikimbizwa na malaika wa Yawe!


Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.


Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza, miji ya mataifa kali itakuogopa.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


ni kama joto la jua juu ya inchi kavu. Lakini wewe unakomesha fujo ya wageni. Kama wingu linavyofifisha joto la jua, ndivyo unavyokomesha nyimbo za ushindi za watu wakali.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Basi, zambi hii itakuwa kwenu kama ufa mukubwa katika ukuta murefu; utabomoka mara moja na kuanguka chini kwa rafla.


Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu; farasi wao nao ni nyama tu, si roho. Yawe akiunyoosha mukono wake, taifa linalotoa musaada litajikwaa, na lile linalosaidiwa litaanguka; yote mawili yataangamia pamoja.


Hapo Waasuria watauawa kwa upanga, lakini si upanga wa watu; wataangamizwa kwa upanga ambao ni zaidi ya ule wa wanadamu. Waasuria watakimbia na vijana wao watatumikishwa kazi za kitumwa.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Kwake mataifa ni kama tone la maji katika mbeketi, ni kama mavumbi juu ya kilo. Kwake visanga ni vyepesi kama mavumbi laini.


Kweli! Wote waliokukasirikia, watapata haya na kufezeheka. Wote wanaopingana nawe, watakuwa wa bure na kuangamia.


Nitawafanya mukuwe kama chombo cha kupepeta, chenye meno mapya na makali. Mutaipepeta milima na kuipondaponda; mutavisagasaga vilima kama maganda.


Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.


Lakini hasara itakupata ambayo hautaweza kujiepusha nayo. Magumu yatakutokea ambayo hautaweza kuyapinga; maangamizi yatakufikia kwa rafla ambayo haujapata kuyaona hata kidogo.


Nilitangaza zamani matukio ya mbele, niliyatangaza mimi mwenyewe na kuyafanya yajulikane kwenu. Mara moja nikaanza kuyatimiza, nayo yakapata kutukia.


Yeye ndiye anayewaangamiza wenye nguvu, na kuziharibu kuta zao zenye nguvu.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ