Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 28:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Wao wananichekelea na kuuliza: Huyu nabii anataka kufundisha nani? Anazani atatuelezea sisi ujumbe wake? Sisi ni watoto wachanga walioachishwa kunyonya juzijuzi?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 28:9
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini nafsi yangu imetulia na kuwa na amani, kama mutoto muchanga anavyotulia na mama yake; ndivyo nafsi yangu inavyokuwa na utulivu.


Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.


“Muliyachukia maarifa, wala hamukuchagua kumwogopa Yawe,


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Mutu huyo anajua kufanya vile, kwa sababu Mungu wake anamufundisha.


Ingawa Bwana atawakulisha chakula cha taabu na kuwakunywesha maji ya mateso, yeye ndiye Mwalimu wenu na hatajificha tena; nanyi mutamwona kwa macho yenu wenyewe.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mukombozi wako, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe, Mungu wako; ninayekufundisha kwa faida yako na kukuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Ni nani aliyeamini mambo tuliyoyasikia? Mukono wa Mungu umefunuliwa kwa ajili ya nani?


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwenda uwaambie watu wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema hivi: Ninyi hamuwezi kupokea mafundisho na kusikia maneno yangu? –Ni ujumbe wa Yawe!


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Nitaongea na nani nipate kumwonya, kusudi wapate kunisikia? Angalia, masikio yao yameziba, hawawezi kusikia ujumbe wako. Maneno ya Yawe, yamegeuka kwao jambo la kuchekelea. Hawalifurahii hata kidogo.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Kweli ninawaambia ninyi: mutu yeyote asiyepokea Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo, hawezi kuingia ndani yake hata kidogo.”


kusudi maneno haya yaliyosemwa na nabii Isaya yatimie: “Bwana, ni nani aliyeamini habari tuliyopasha? Nani aliyefunuliwa matendo ya uwezo ya Bwana?”


Hukumu inatokana na hivi: mwangaza umekuja katika ulimwengu, lakini watu wanapenda giza kuliko mwangaza, kwa sababu matendo yao ni mabaya.


Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ