Musa akamwita Bezaleli na Oholiabu na kila mutu ambaye alikuwa amejaliwa ujuzi na Yawe na kila mutu ambaye moyo wake ulimusukuma kufanya kazi kwa nia nzuri.
Hapana! Akisha kusawanisha shamba lake, anapanda mbegu za kunde na mbegu za vikolezo, anapanda ngano na shayiri kwa mustari, na kwenye mipaka ya shamba mimea mingine.
Wao wananichekelea na kuuliza: Huyu nabii anataka kufundisha nani? Anazani atatuelezea sisi ujumbe wake? Sisi ni watoto wachanga walioachishwa kunyonya juzijuzi?
Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.