Isaya 28:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
25 Hapana! Akisha kusawanisha shamba lake, anapanda mbegu za kunde na mbegu za vikolezo, anapanda ngano na shayiri kwa mustari, na kwenye mipaka ya shamba mimea mingine.
Wewe utwae ngano, shayiri, mahalagi, manjegere, mutama na ulezi, uvitie vyote katika chombo kimoja, ujitengenezee mukate. Mukate huo ndio utakaokuwa chakula chako wakati unapolala kwa upande mumoja, siku zote mia tatu na makumi kenda.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula, lakini mumeacha mambo makubwa yanayoamuriwa na Sheria, kama vile haki, huruma, na uaminifu. Mambo hayo ndiyo muliyopaswa kushika pasipo kuacha mengine.