Basi wajumbe wale wakaenda toka muji mumoja mpaka mwingine katika inchi yote ya Efuraimu na Manase, wakafika hata katika inchi ya Zebuluni. Lakini watu waliwacheka na kuwazarau.
Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.
Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.
Musa akamujibu: “Mara tu nitakapokuacha, kesho nitamwomba Yawe makundi haya ya mainzi yatoweke kwako wewe mufalme, wakubwa wako na watu wako. Lakini wewe usitudanganye tena kwa kukataa kuwaacha watu kwenda kutoa sadaka kwa Yawe.”
Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.
Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.
Yehudi alipokuwa amekwisha kusoma vipindi vitatu au vine hivi vya kitabu kile, mufalme alivikatakata kwa kisu na kuvitupa katika moto wa makaa. Aliendelea kufanya hivyo mpaka kitabu chote kikateketezwa.
Aliyahesabu makosa yangu yote akayakusanya pahali pamoja; aliyafunga katika shingo langu kama nira, nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake. Yawe aliniweka katika mikono ya watu ambao siwezi kuwapinga.
Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”