Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 28:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Maana Yawe atasimama kama kule kwenye mulima Perasimu; atawaka hasira kama kule katika bonde la Gebeoni. Atatimiza mupango wake wa ajabu; atatenda kazi yake ya ajabu sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 28:21
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Daudi akafika Bali-Perasimu na kuwashinda Wafilistini. Halafu akasema: “Yawe amepita katikati ya waadui zangu kama mafuriko ya maji yanayoenda mbio.” Kwa hiyo pahali pale pakaitwa “Bwana Anayepita Katikati”.


Daudi alifanya kama vile alivyoamuriwa na Yawe, naye akawapiga Wafilistini kutokea Geba mpaka Gezeri.


Basi, Daudi akaenda kule Bali-Perasimu, akawashinda; halafu akasema: “Mungu amebomoa ukingo wa waadui zangu kwa mukono wangu, kama mafuriko ya maji yanayoenda mbio.” Kwa hiyo pahali pale panaitwa “Bwana Mwenye Kubomoa.”


Daudi akafanya kama vile alivyoamuriwa na Mungu. Akawapiga waaskari wa Wafilistini kutokea Gibeoni mpaka Gezeri.


Nani aliyenisaidia kumupinga mutu mwovu? Nani aliyekuwa upande wangu juu ya wabaya?


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Kila mara itakapopita kwenu itawapata; nayo itapita kila asubui, muchana na usiku. Kusikia ujumbe huu tu kutakuwa kitisho.


Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu, mambo ya ajabu na ya kushangaza. Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima, na akili ya wenye akili wao itatoweka.


Watakapowaona watoto wao, watoto niliowajalia mimi mwenyewe, watalitukuza jina langu mimi Mutakatifu wa Yakobo, watakuwa na heshima kwangu mimi Mungu wa Israeli.


Wakati ulipotenda maajabu ambayo hatukutazamia, ulishuka chini nayo milima ikatetemeka ilipokuona.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Wapenzi wako wote wamekusahau; hawajali kitu chochote juu yako. Nimekupiga sawa vile ungekuwa adui yangu. Umeazibiwa bila huruma, kwa sababu kosa lako ni kubwa, zambi zako ni nyingi sana.


Wapita njia wote wanakuchekelea; wanakupigia muunzi, ee Yerusalema, wakitikisa vichwa vyao kwa mazarau na kusema: Huu ndio ule muji uliofikia ukamilifu wa uzuri, muji uliokuwa furaha ya dunia nzima?


Yeye hapendelei kuwatesa wala kuwahuzunisha wanadamu.


Siku ya tano ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi na mbili tangu tulipopelekwa katika uhamisho, mutu mumoja aliyetoroka kutoka Yerusalema alikuja kwangu, akasema: Muji Yerusalema umetekwa!


Mungu akasema: Muangalie mataifa, muone! Mustaajabu na kushangaa. Maana ninatenda kitu ukiwa bado unaishi, kitu ambacho ungeambiwa haungesadiki.


Naye Yawe akawatia hofu kubwa mbele ya Waisraeli ambao waliwaua watu wengi kule Gibeoni wakiwakimbia kwenye njia ya muteremuko wa Beti-Horoni mpaka Azeka na Makeda ambako vilevile waliwaua watu wengi sana.


Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.


Wakati Yawe alipowatia Waamori katika mikono ya Waisraeli, Yoshua alimwomba Yawe mbele ya Waisraeli wote, akasema: “Wewe jua, simama kimya juu ya Gibeoni, wewe mwezi, katika bonde la Ayaloni.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ