Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!
Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.
Vilevile kwa nafasi hii nitaivuruga mipango ya watu wa Yuda na ya watu wa Yerusalema. Nitawatoa washindwe na kuuawa kwa panga na waadui zao, wale wanaovizia maisha yao. Nazo maiti zao nitaziacha kuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.
Ni wachache tu ndio watakaoponyoka katika vita na kurudi kutoka inchi ya Misri na kwenda katika inchi ya Yuda. Halafu Wayuda wote waliobaki kati ya wale waliokwenda kukaa Misri watatambua ni neno la nani lenye nguvu: langu au lao!
Yawe anasema hivi: Maji yanapanda kutoka kaskazini, nayo yatakuwa muto uliofurika; yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake, muji na wakaaji na wanaoishi humo. Watu watalia, wakaaji wote wa inchi wataomboleza.
Lakini yule mufalme mupya alimwasi mufalme wa Babeli kwa kuwatuma wajumbe Misri kuomba farasi na waaskari wengi. Mufalme huyo atashinda? Anayefanya hivyo na kuvunja agano lake ataweza kuepuka azabu?
Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.
Babu zenu hawakupata azabu kwa sababu ya kukataa maagizo yangu na amri nilizowapa kwa njia ya watumishi wangu manabii? Wakati huo, wao waligeuka na kusema kwamba: Yawe wa majeshi alikusudia kututendea kulingana na mienendo yetu na matendo yetu, na kweli ndivyo alivyotutendea.