Isaya 28:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.
Nitauazibu Yerusalema kama vile nilivyofanya Samaria, na mufalme Ahabu na wazao wake. Nitasafisha Yerusalema kama vile wanavyosafisha sahani na kuigeuza kisha kusafishwa.
Maana, hata kama sasa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaorudi. Maangamizi yamepangwa yafanyike, nayo yatafanyika kwa haki tu.
Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;
Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!
Bwana amejichagulia mutu wake shujaa na mwenye nguvu, ambaye ni kama mvua ya mawe na zoruba kali, kama zoruba ya mafuriko makubwa; kwa mukono wake atawatupa chini.
Pumzi yake ni kama mafuriko ya muto ambao maji yake yanafika mpaka kwenye shingo. Anakuja kupepeta mataifa kwa lungo ya maangamizi, kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.
Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.
Vilevile kwa nafasi hii nitaivuruga mipango ya watu wa Yuda na ya watu wa Yerusalema. Nitawatoa washindwe na kuuawa kwa panga na waadui zao, wale wanaovizia maisha yao. Nazo maiti zao nitaziacha kuwa chakula cha ndege na nyama wa pori.
Kwa hiyo, kama vile nilivyoutendea muji wa Shilo, ndivyo nitakavyolitendea hekalu hili linalojulikana kwa jina langu, hekalu ambalo ninyi munalitegemea; ndiyo pahali hapa ambapo niliwapa ninyi na babu zenu.
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.
Nitamwazibu Gogi kwa ugonjwa mukali na mauaji. Nitanyesha mvua nyingi na mvua ya mawe na moto na kiberiti juu yake, juu ya makundi yake, na mataifa yale mengi yanayokuwa pamoja naye.
Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.
Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.
Kisha mvua ya mawe makubwa yenye uzito wa zaidi ya kilo makumi ine ikanyesha juu ya watu. Nao wakamutukana Mungu kwa sababu ya hilo pigo la mvua ya mawe, kwa maana pigo lile lilileta hasara kubwa sana.
Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”
Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.