Basi Yawe atawafundisha kama watoto wadogo: kanuni juu ya kanuni, mustari juu ya mustari; mara hiki, mara hiki! Nao watalazimishwa kukimbia lakini wataanguka machalichali, watavunjika, watanaswa na kutekwa.
Kwa kumaliza, wandugu zangu, mufurahi kwa ajili ya kuungana kwenu na Bwana. Hainiuzi kitu kuwaandikia tena maneno yale yale niliyowaandikia mbele. Hayo yote ni kwa ajili ya kuwakingia hatari.
Kweli, kwa wakati huu, ninyi mungepaswa sasa kuwa walimu, lakini mungali munahitaji kufundishwa tena mafundisho ya mwanzo ya neno la Mungu. Mumegeuka tena wenye kuhitaji kunywa maziwa, wala si chakula kigumu.