Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 27:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 27:13
51 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Sebania, Yosafati, Netaneli, Amasai, Zekaria, Benaya na Eliezeri, waliokuwa makuhani, waliwekwa kwa kupiga baragumu mbele ya Sanduku la Agano. Obedi-Edomu na Yehiya waliwekwa vilevile kuwa walinzi wa sanduku.


Ametuchagulia inchi hii ikuwe urizi wetu, ambayo ni utukufu wa Yakobo anayemupenda.


muvumishe wimbo wa shangwe, mupige ngoma, mucheze zeze na kinubi cha sauti nzuri.


Haki na sheria ndio musingi wa utawala wako; wema na uaminifu vinakutangulia!


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.


Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria kwa ajili ya watu wake waliobaki humo kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wakati walipotoka katika inchi ya Misri.


Enyi wakaaji wote katika ulimwengu, nanyi munaojaza dunia! Bendera itakaposimikwa kwenye mulima, muangalie! Baragumu itakapopigwa, musikilize.


Yawe atajijulisha kwa Wamisri na hapo ndipo Wamisri watakapomwitikia na kumwabudu kwa kumutolea matoleo na sadaka za kuteketezwa. Vilevile watafanyia Yawe viapo ambavyo watavitimiza.


Yawe atawaazibu Wamisri na kuwaponya. Nao watamurudilia, naye atayasikiliza maombi yao na kuwaponya.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Juu ya mulima Sayuni, Yawe wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya nyama zenye kunona na divai nzuri, nyama tamu zenye mafuta, pamoja na divai safi.


Nitaiambia kaskazini: “Uwaache waondoke”, na kusini: “Usiwazuize! Muwarudishe watu kutoka mbali, kutoka kila pahali katika dunia.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.


Ninayajua matendo yao na mawazo yao. Ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na wa luga zote, wakusanyike pamoja na kuuona utukufu wangu.


Katika kila sikukuu ya mwandamo wa mwezi, na katika kila siku ya Sabato, wanadamu wote watakuja kuniabudu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Maana kutakuja siku ambapo walinzi watalalamika hivi katika vilima vya Efuraimu: Musimame, tupande kwenda Sayuni kwa Yawe, Mungu wetu.


Wakaenda katika inchi ya Misri, wakafika katika muji wa Tapanesi. Ndivyo walivyokataa kutii maneno ya Yawe.


Ni wachache tu ndio watakaoponyoka katika vita na kurudi kutoka inchi ya Misri na kwenda katika inchi ya Yuda. Halafu Wayuda wote waliobaki kati ya wale waliokwenda kukaa Misri watatambua ni neno la nani lenye nguvu: langu au lao!


Nitawatoa kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka katika inchi mulimosambazwa kwa mukono wangu wenye nguvu, kwa ukali na kwa kasirani yangu.


Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitawahurumia Waisraeli wazao wa Yakobo, na kuwarudishia fanaka yao. Ninataka jina langu takatifu liheshimiwe siku zote.


Zaidi ya hayo, atapiga mahema yake makubwa kati ya bahari na mulima mutukufu na mutakatifu. Lakini atakuwa amefikia ukomo wake, na hakutakuwa mutu yeyote wa kumusaidia.


Watakuja kutoka Misri wakitetemeka kama ndege, wataruka kutoka Asuria kama njiwa nami nitawarudisha kwao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Hawatakaa katika inchi ya Yawe. Watu wa Efuraimu watarudi katika utumwa kule Misri. Watakula vyakula vichafu kule Asuria.


Kisha, katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ambayo ni siku ya kufanyiwa upatanisho mutatuma mutu kupiga baragumu katika inchi yote.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Kisha, kila mutu aliyebaki kati ya mataifa yote yaliyokuja kuushambulia Yerusalema, atakuwa akikuja Yerusalema mwaka kwa mwaka, kwa kumwabudu Yawe wa majeshi anayekuwa mufalme, na kushiriki kwa sikukuu ya Vibanda.


Yawe anasema hivi: Nitawaokoa watu wangu kutoka inchi ya mashariki na kutoka inchi ya magaribi


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.


“Roho wa Bwana yuko pamoja nami, maana amenichagua niwahubirie wamasikini Habari Njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kwamba watakombolewa nao vipofu kwamba wataona. Amenituma kuwapa wanaoteswa uhuru,


Basi ninauliza: hawakusikia habari hii? Ndiyo, wameisikia! Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Sauti yao imesikilika katika dunia yote, maneno yao yamefika pande zote za dunia.”


Kwa sababu amri itakapotoka na sauti ya malaika mukubwa itakaposikilika, na baragumu ya Mungu itakapolia, Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni. Halafu wale waliokufa wakimwamini Kristo watafufuliwa kwanza.


Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.


Lakini wakati malaika wa saba atakapopiga baragumu, Mungu atatimiza mipango yake aliyoficha sawa vile alivyotangaza kwa kinywa cha manabii waliomutumikia.


Kisha nikaona wamalaika saba wakisimama mbele ya Mungu, nao wakapewa baragumu saba.


Wale wamalaika saba waliokuwa na baragumu saba wakajitayarisha kwa kuzipiga.


Sauti ile ikamwambia yule malaika wa sita aliyeshika baragumu hivi: “Uwafungue wale wamalaika wane waliofungwa kwenye muto mukubwa Furati.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ