Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 27:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Siku hiyo, Yawe atapepeta ngano yake kutokea kwenye muto Furati mpaka kwenye mupaka wa Misri, nanyi Waisraeli mutakusanywa mumojamumoja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 27:12
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na Waisraeli wote. Nao walitoka tangu kwenye kiingilio cha Hamati, mpaka muto wa Misri.


Lakini mukinirudilia, mukishika amri zangu na kuzifuata hata ingawa nitakuwa nimewatawanya mbali kabisa, nitawarudisha pahali nilipochagua kuwa pahali pangu pa kuabudiwa.’


Mungu ataviponda vichwa vya waadui zake, ndivyo vichwa vya wanaoendelea katika njia mbaya.


Atawale kutoka bahari hata bahari, kutoka muto Furati hata miisho ya dunia.


Watabaki wachache kama vile kisha kuangusha matunda ya mizeituni: matunda mawili au matatu katika tawi la juu; mane, matano katika matawi yanayozaa sana. –Ni ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli.


Lakini sasa Yawe anasema. Aliniita tangu katika tumbo la mama kusudi nipate kuwa mutumishi wake, nilirudishe taifa la Yakobo kwake na kukusanya wazao wa Israeli kwake. Yawe amenijalia heshima mbele yake. Mungu wangu amekuwa nguvu yangu.


–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, maana, mimi ndimi Bwana wenu. Nitawatwaa mumoja kutoka kila muji, na wawili kutoka katika kila ukoo, niwapeleke mpaka kwenye mulima Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ni wachache tu ndio watakaoponyoka katika vita na kurudi kutoka inchi ya Misri na kwenda katika inchi ya Yuda. Halafu Wayuda wote waliobaki kati ya wale waliokwenda kukaa Misri watatambua ni neno la nani lenye nguvu: langu au lao!


Nitawatoa kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka katika inchi mulimosambazwa kwa mukono wangu wenye nguvu, kwa ukali na kwa kasirani yangu.


Kisha kuwatoa toka katika inchi ambako mumesambazwa na kuwakusanya pamoja, nitazipokea sadaka zenu zenye harufu nzuri. Nami nitaonyesha utakatifu wangu kati yenu mbele ya mataifa mengine.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitawahurumia Waisraeli wazao wa Yakobo, na kuwarudishia fanaka yao. Ninataka jina langu takatifu liheshimiwe siku zote.


Upande wa kusini, toka Tamari mupaka utaendelea mpaka kwenye chemichemi ya Meriba-Kadesi. Kutoka Meriba-Kadesi mupaka utaelekea kusini magaribi mpaka bahari ya Mediteranea ukipitia upande wa mashariki ya inchi ya Misri.


Nitatoa amri, na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifa kama mutu anavyopepeta ngano kusudi niwatoshe wote wasiofaa.


Yawe anasema hivi: Nitawaokoa watu wangu kutoka inchi ya mashariki na kutoka inchi ya magaribi


“Ni nani kati yenu akiwa na kondoo mia moja, na mumoja wao akipotea, atakayekosa kuwaacha wale wengine makumi tisa na tisa kwenye mashamba ya kulishia wanyama na kwenda kumutafuta yule aliyepotea mpaka atakapomupata?


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.


Kutoka hapo ulipita karibu na Asimoni na kufuata kijito cha Misri mpaka kufikia kwenye bahari ya Mediteranea. Hapo ndipo mupaka wa kusini wa Yuda ulipopita.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ