Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 26:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 26:8
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


Heri wale wanaofuata sheria ya Mungu, wanaotenda siku zote mambo ya haki.


Ninamutumainia Yawe kwa moyo wangu wote. Ninaaminia sana neno lake.


Nimeshika maagizo yake yote, sikuacha kufuata masharti yake.


Kama pongo anavyotamani maji ya kijito, ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!


Kwa matendo yako makubwa unatuitikia na kutuokoa, ewe Mungu mwokozi wetu. Wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote katika dunia yote na mbali katika bahari.


Mbinguni, nani anayeweza kunisaidia isipokuwa wewe? Na katika dunia hamuna ninachokitamani isipokuwa wewe!


Ee Yawe wa majeshi, kweli makao yako yanapendeza!


Uwaambie Waisraeli kwamba: Yawe, Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutuma kwao. Hili ndilo jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote.


Ninawasihi, enyi wabinti wa Yerusalema, mukimwona mupenzi wangu, mumwelezee kwamba ninaugua kwa ajili ya mapenzi!


Siku hiyo mutasema: Mumushukuru Yawe, muombe kwa jina lake. Mujulishe kwa mataifa matendo yake, mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.


na wale wa upande wa mashariki wanamusifu. Watu wa mbali wanalisifu jina la Yawe, Mungu wa Israeli.


Wewe, ee Yawe, ndiwe Mungu wangu; nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana umetenda mambo ya ajabu; unaitimiza kwa uaminifu na kweli mipango uliyoipanga tangu zamani.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Ee Yawe, Mungu wetu, tulipata kutawaliwa na wabwana wengine ambao si wewe, lakini tunakubali wewe pekee kuwa Mungu wetu.


Hata hivyo, Yawe anangoja kuwasamehe, atasimama na kuwaonea huruma. Yawe ni Mungu wa haki. Heri wote wale wanaomutumainia.


Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Munisikilize, enyi watu wangu, munitegee sikio, enyi taifa langu. Sheria na haki zitatoka kwangu mimi; nazo zitakuwa mwangaza wa mataifa.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki, maana ninakaribia kuwaokoa, watu wataona wazi kwamba ninawakomboa.


Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Hizo ndizo amri na maagizo ambayo Yawe aliwapa Waisraeli kwa njia ya Musa katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na muji wa Yeriko.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Siku moja alipokuwa akikusanyika pamoja nao, akawaagiza: “Musitoke Yerusalema, lakini mubaki kule mukingojea zawadi ambayo Baba yangu aliahidi, ile niliyowaambia ninyi.


Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu.


Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ