Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 26:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu, mujifungie humo ndani. Mujifiche kwa muda mufupi, mpaka kasirani ya Yawe ipite.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 26:20
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.


Kila aina yao waliingia dume na dike kama vile Mungu alivyomwamuru Noa. Kisha, Yawe akafunga mulango wa chombo nyuma ya Noa.


Heri ungenificha katika kuzimu, ungenificha mpaka kasirani yako itulie, nawe ungenipimia muda kwa kunikumbuka tena.


Uniokoe, ee Yawe, kutoka waadui zangu, maana ninakimbilia kwako.


Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche chini ya kivuli cha mabawa yako,


Siku ya taabu atanificha ndani ya nyumba yake; atanificha katika hema lake, atanilinda salama juu ya mulima.


Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake; mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.


Kweli, mazuri yako ni mengi sana, unayowawekea wale wanaokuabudu! Unawatendea mazuri mbele ya watu wote wale wanaokukimbilia.


Wewe unanificha kwa kunilinda wakati wa taabu. Ninazungukwa na ukombozi wako.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi alipomuponyoka Saulo na kujificha katika pango.


Unihurumie, ee Mungu, unihurumie, maana ninakukimbilia wewe. Ninakimbilia kwenye kivuli cha mabawa yako, mpaka zoruba ya maangamizi ipite.


Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa, ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,


Atakufunika kwa mabawa yake; utapata usalama kwake. Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.


kusudi siku ya taabu apate utulivu, mpaka waovu wachimbiwe shimo.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.


Maana bado kidogo, nayo hasira yangu itapita na kasirani yangu itawageukia Waasuria.


Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!


Wanakuja kutoka inchi za mbali, wanatoka hata miisho ya dunia: Yawe na silaha za hasira yake anakuja kuiangamiza dunia.


Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.


Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.


Munisikilize, enyi watu wangu, munitegee sikio, enyi taifa langu. Sheria na haki zitatoka kwangu mimi; nazo zitakuwa mwangaza wa mataifa.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Nitawashibisha makuhani kwa nyama wenye kunona, watu wangu watatosheka kwa wema wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini niliwapa amri kwamba waitii sauti yangu kusudi nikuwe Mungu wao, nao wakuwe watu wangu. Niliwaamuru vilevile waishi kama nilivyowaagiza, kusudi wapate uheri.


Lakini, uwaambie hao wanaokuwa katika uhamisho kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Ingawa nimewapeleka mbali kati ya mataifa na kuwasambaza katika inchi zingine, hata hivyo, mimi nipo pamoja nao huko wanakokuwa, kama vile hekalu kwao.


Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ