Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 26:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mufungue milango ya muji, taifa aminifu liingie; taifa linalotenda mambo ya haki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 26:2
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

kusudi niweze kuona uheri wa wachaguliwa wako, nipate kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuona utukufu pamoja na watu wako.


Munifungulie milango ya watu wa haki, niingie na kumushukuru Yawe!


Huu ndio mulango wa Yawe, watu wa haki watapitia humo.


Mufunguke, enyi milango; mufunguke, enyi milango ya tangia zamani, kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.


Mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”


Lakini wazao wa Israeli watapata ushindi toka kwa Yawe na kufurahi.


Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mukifanya hivyo mutaonekana kama mwangaza wa mapambazuko, na mutapona haraka. Matendo yenu mema yatawatangulia, nami nitawalinda kutoka nyuma kwa utukufu wangu.


Milango yako itakuwa wazi siku zote; usiku na muchana haitafungwa, kusudi watu wakuletee utajiri wa mataifa, pamoja na wafalme wao katika maandamano.


Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Kwa ajili ya Sayuni sitakaa kimya, kwa ajili ya Yerusalema sitatulia, mpaka kuokolewa kwake kuonekane kama umeme, wokovu wake utokee kama mwangaza.


Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.


Mataifa watauona wokovu wako, wafalme wote watauona utukufu wako. Nawe utaitwa kwa jina jipya ambalo litapangwa na Yawe mwenyewe.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Watu wengi wa mataifa ya kigeni na wakaaji wa miji mingi watajaa katika Yerusalema.


Nao walisifu Mungu na kufurahiwa na watu wote. Na kila siku Bwana aliongeza katika kundi la waamini watu waliokuwa wakiokolewa.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Lakini, kufuatana na ahadi ya Mungu, tunangojea kwamba kutakuwa mbingu mupya na dunia mupya, pahali haki itakapokuwa.


Wapendwa wangu, wakati nilipokuwa nikifanya bidii sana ya kuwaandikia juu ya wokovu tunaoshiriki wote pamoja, nikaona sherti niwaandikie na kuwaonya mupate kutetea imani ile Mungu aliyotoa mara moja tu kwa watu wake.


Kwa hiyo watu wa mataifa watatembea katika mwangaza wake na wafalme wa dunia wataleta utajiri wao ndani yake.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ