Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 25:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 25:8
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ameniokoa toka kifo na kufuta machozi yangu; akanilinda nisianguke.


Nimekuwa mugeni kwa wandugu zangu, kaka na dada zangu hawanitambui.


Wafu wako wataishi tena, miili yao itafufuka. Wanaolala katika mavumbi wataamuka na kuimba kwa furaha! Mungu atapeleka umande wake wa uzima, nao wanaokuwa kwa wafu watatoka wazima.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa, na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Kwa vile mulipata haya mara mbili, watu wakaona kwamba mazarau ni majaliwa yenu, sasa mutapata sehemu mara mbili kuwa mali yenu, na furaha yenu itadumu milele.


Nami nitaufurahia Yerusalema, nitawafurahia watu wangu. Sauti ya kilio haitasikilika tena, kilio cha taabu hakitakuwa tena.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Yawe anasema hivi: Acha kulia, panguza machozi yako, maana utapata malipo kwa kazi yako. –Ni ujumbe wa Yawe.– Watoto wenu watarudi kutoka inchi ya waadui zenu.


Inanipasa kuwakomboa hawa watu kutoka kuzimu; sharti niwaokoe kutoka kifo! Ewe kifo, mapigo yako ni wapi? Ewe kuzimu, kuangamiza kwako ni wapi? Mimi sitawaonea tena huruma!


“Sasa Bwana amenifanyia mema kwa kunitendea hivi; ameniondolea haya ya kutokuzaa niliyokuwa nayo mbele ya watu.”


Na wakati mwili huu wa kuharibika utakapovaa ule wa kutoharibika, nao mwili wa kufa utakapovaa ule wa kutokufa, halafu Maandiko Matakatifu haya yatatimia: “Kifo kimekomeshwa; kimeshindwa kabisa.”


Lakini neema hii imeonekana sasa kwa kuja kwa Mwokozi wetu Kristo Yesu. Yeye ameshinda nguvu za lufu na kwa njia ya Habari Njema ameonyesha wazi uzima wa milele.


Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.


Kisha kifo na kuzimu vikatupwa katika ziwa la moto. Ziwa lile la moto ndicho kifo cha pili.


Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.”


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ