Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 25:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Juu ya mulima Sayuni, Yawe wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya nyama zenye kunona na divai nzuri, nyama tamu zenye mafuta, pamoja na divai safi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 25:6
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kweli wema wako ni bora! Wanadamu wanakimbilia kwenye kivuli cha mabawa yako.


Nitakushukuru maisha yangu yote, nitakuomba nikikuinulia mikono yangu.


Lakini alichagua kabila la Yuda, mulima Sayuni anaoupenda.


Heri midomo yako ingalinibusu, maana mapendo yako ni bora kuliko divai.


Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Mukiwa tayari kunitii, mutakula mazao mema ya inchi.


Yawe ataulinda mulima wa Sayuni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa ndani ya inchi yao kama nyasi katika shimo la mboleo.


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika mutungi. Hajamimiliwa toka chombo kimoja katika chombo kingine, hajapata kupelekwa katika uhamisho. Kwa hiyo angali na onjo yake, harufu yake nzuri haijabadilika hata kidogo.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Nami ninawaambia kwamba tangia sasa sitakunywa tena divai mpaka siku ile nitakapoikunywa mupya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”


Ninawaambia wazi kwamba watu wengi watakuja toka mashariki na magaribi, nao watachangia meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwenye karamu katika Ufalme wa mbinguni.


Kisha akawaambia: “Mwende katika dunia yote na kuhubiri Habari Njema kwa kila mutu.


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Hakuna mutu aliyekwisha kunywa divai ya zamani atakayetaka tena divai mupya. Kwa maana anasema kwamba ile ya zamani ni nzuri zaidi.”


Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.


Halafu malaika akaniambia: “Andika maneno haya: Heri wale wanaoalikwa kwa karamu ya ndoa ya Mwana-Kondoo.” Naye akasema tena: “Maneno haya ni ya kweli yanayotoka kwa Mungu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ