Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 25:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 25:4
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini aliwaokoa wakosefu katika taabu zao, akaongeza jamaa zao kama kundi la kondoo.


Ninashikamana na maagizo yako, ee Yawe; usikubali nipatishwe haya!


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Yawe ni mulinzi wako; yuko upande wako wa kuume kwa kukukinga.


Nitamwambia Yawe kwa moyo wangu wote: “Wewe, ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe! Wewe unawaokoa wamasikini kutoka makucha ya wenye nguvu, wamasikini na wakosefu kutoka mikono ya wanyanganyi.”


ningesafiri mbali sana, ningepata makao katika jangwa,


Atawahurumia wazaifu na wakosefu, atayaokoa maisha yao wenye shida.


Mufalme awatetee wamasikini wa taifa, awasaidie wakosefu, na kuwaangamiza watesaji.


Yawe ni kikingio cha watu wanaoonewa; yeye ni kikingio katika nyakati za taabu.


Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa, ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,


Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.


Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.


Wamoabu wanawaambia watu wa Yuda: Mutuongoze, mutuamue. Mueneze ulinzi wenu juu yetu, kama vile usiku unavyoeneza kivuli chake. Mutufiche sisi wakimbizi; musitutoe sisi tuliofukuzwa.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Wakitaka ulinzi wangu, basi, wafanye amani nami. Wafanye amani nami!


Atawaongoza waamuzi wa tribinali kuhukumu kwa haki, nao walinzi wa muji atawapa nguvu.


Wanyenyekevu watapata furaha mupya kwa Yawe, na wamasikini kati ya watu watashangilia kwa furaha, kwa sababu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Kundi la waadui zako litakuwa kama mavumbi laini, waliokutendea ukali watakuwa kama maganda. Hayo yatafanyika kwa rafla.


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Mutu wa namna hiyo anaishi kwenye nafasi ya juu, pahali salama, penye pango na mawe makubwa; atapewa chakula chake siku zote, na maji yake ya kunywa hayatakosekana.


Ee Yawe, utuonee huruma, kwako tumeliweka tumaini letu. Ukuwe kikingio chetu kila siku, mwokozi wetu wakati wa taabu.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Yawe anasema hivi: Kweli! Hata mateka za shujaa zitarudishwa, wafungwa wa mutu mutesaji wataokolewa. Mimi mwenyewe nitawapiganisha waadui zako, mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.


Mutakapolia kwa kuomba musaada, basi ile lundo ya sanamu zenu iwaokoe! Upepo utavipeperushia mbali; pumzi itavitupilia mbali. Lakini watakaotafuta kimbilio kwangu, watarizi inchi, mulima wangu mutakatifu utakuwa mali yao.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Mimi nitakuwa kimbilio. Nitakuwa vilevile kama jiwe la kujikwaa, jiwe kubwa la kuziangusha falme za Israeli na Yuda. Nitakuwa mutego wa kuwatega na kuwanasa wakaaji wa Yerusalema.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Utakwenda mbio kama zoruba na kuifunika inchi kama wingu, wewe mwenyewe na kundi lako lote la waaskari pamoja na mataifa mengi yanayokuwa pamoja nawe.


Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ