Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 25:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 25:2
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akibomoa, hakuna anayeweza kujenga upya; akifunga mutu, hakuna anayeweza kumufungua.


Hautakaliwa tena na watu hata kidogo, watu hawataishi humo katika vizazi vyote. Hakuna Mwarabu atakayesimamisha hema yake humo, wala muchungaji atakayechunga nyama wake humo.


Pahali pake ni nyama wakali wa pori ndio watakuwa ndani yake, bundi watajaa katika nyumba zake. Mbuni wataishi humo, pepo watachezea huko.


Fisi watalia ndani ya pango zake, mbweha wataonekana ndani ya nyumba zao za raha. Wakati wa Babeli umekaribia, wala siku zake hazitaongezwa.


Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa tingitingi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki. Damasiki utakoma kuwa muji; utakuwa lundo la mabomoko.


Pango za Efuraimu zitatoweka, na utawala wa Damasiki utakwisha. Waaramu ambao watabaki wazima, hawatakuwa na utukufu zaidi kama wazao wa Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Angalia, wanakuja: waaskari wapanda-farasi wawiliwawili. Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka! Sanamu zote za miungu yake zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!


Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.


(Ni Wakaldea, wala si Waasuria, waliowaacha nyama wa pori waushambulie muji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia muji huo minara ya kuushambulia, wakabomoa nyumba zake na kuufanya mabomoko.)


Muji wa fujo umejaa uharibifu; kila nyumba imefungwa kusudi mutu asiingie.


Atabomoa pango za miji ya Moabu yenye kuta ndefu na kuiangusha chini ndani ya mavumbi.


Amewaporomosha waliokaa pande za juu, muji wenye utukufu ameuangusha mpaka chini, ameutupa mpaka katika mavumbi.


Muji ule wenye kuta sasa umekuwa mutupu, umeachwa na kuhamwa kama jangwa, humo ngombe wanakula na kupumzika.


Maana nyumba ya kifalme itaachwa ukiwa, muji huo wa watu wengi utahamwa. Mulima na munara wa ulinzi utakuwa mapango milele, punda wa mwitu watapitapita huko kwa furaha, kondoo watapata malisho yao humo.


Lakini mvua ya mawe itanyesha na kuangusha pori, na muji wake utaangamizwa.


Miiba itaota katika pango zake, miiba na michongoma ndani ya kuta zake. Itakuwa makao ya imbwa wa pori, nafasi ya mbuni.


Haujasikia, ewe Saniharibu, kwamba mimi Yawe nilipanga jambo hili tangu zamani? Ninachotimiza sasa nilikipanga zamani. Nilikuweka uifanye miji yenye kuzungukwa na kuta kuwa lundo la mabomoko.


Kwako hakutapatikana jiwe la kujenga, hata jiwe kwa kujenga musingi! Utakuwa kama jangwa milele. –Ni ujumbe wa Yawe!–


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


hakika mutawaua kwa upanga watu wa muji huo. Mutauteketeza kwa upanga kabisa na ngombe wote vilevile.


Wakajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia na kufanya kilio, nao walilalamika, wakisema: “Ole! Ole kwa muji ule mukubwa! Wote wanaokuwa na mashua za kufanya uchuuzi juu ya bahari walijitajirisha na mali zake nyingi. Lakini kwa muda wa saa moja tu umebaki mutupu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ