Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 24:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 24:5
49 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


basi, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitaleta juu ya Yerusalema na Yuda hasara ambayo hata yeyote atakayesikia atashituka.


Nitawatendea hayo yote kwa sababu wameniasi na kunikasirikisha tangia wakati wazee wao walipotoka Misri mpaka leo.”


Lakini Manase aliwapotosha watu wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema, wakatenda maovu zaidi kuliko mataifa ambayo Yawe aliyaangamiza mbele ya watu wa Israeli.


Alimusimamishia Yakobo ahadi yake, akamuhakikishia agano hilo la milele.


Moyo wangu umejaa hofu, vitisho vya kifo vimenisonga.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Barabara kubwa zimebaki tupu; hakuna anayesafiri kupitia ndani yao. Mapatano yanavunjwa ovyo, washuhuda wanazarauliwa. Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.


Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakutendea wewe Yerusalema kama unavyostahili. Wewe umekizarau kiapo, ukivunja agano.


Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.


kwa sababu hawakufuata maagizo yangu, lakini waliyakataa masharti yangu, wakazikufuru Sabato zangu na kuziabudu sanamu za miungu ya wazee wao.


Nitafanya nao agano la amani, nalo litakuwa agano la milele. Nitawabariki na kuwafanya wakuwe wengi, nami nitaweka hekalu langu kati yao milele.


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Tulikataa kukusikiliza, ee Bwana wetu, Mungu wetu; hatukutenda kulingana na sheria zako ulizotupatia kwa njia ya watumishi wako manabii.


Tumetenda zambi, tumekosa, tumetenda maovu na kukuasi. Tumevunja amri zako na maagizo yako.


Lakini mulivunja agano langu kama mulivyofanya katika muji wa Adamu; kule walikosa uaminifu kwangu.


Munapaswa kushika na kutimiza masharti yangu na maagizo yangu yote. Kama sivyo inchi ile ambamo ninawapeleka itawatapika.


Kadiri itakapokuwa katika hali ya ukiwa, itapata sehemu ambayo haikupata katika Sabato zenu mulipokuwa mukiishi mule.


Musimame! Muende! Hapa hakuna tena pahali pa kupumzika! Kwa ajili ya ukosefu wenu wa uaminifu, maangamizi makubwa yanawangojea!


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Watu wa usawa walinona, wakapiga mateke. Walinenepa sana, kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba, wakazarau Mulima wa wokovu wao.


Akasema hivi: Nitawaficha uso wangu nione mwisho wao utakuwa namna gani. Maana wao ni kizazi kipotovu, watoto wasiokuwa na uaminifu wowote.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Katika agano la kwanza wanasema juu ya kanuni za ibada na juu ya nafasi ya kuabudia iliyojengwa na watu.


Kama mukivunja agano la Yawe, Mungu wenu, ambalo aliwaamuru mulishike, mukienda kuitumikia miungu mingine na kuinama mbele yao; basi, hasira ya Yawe itawaka juu yenu, nanyi mutaangamia mara moja kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.”


Hivyo, Yoshua akafanya agano na Waisraeli kule Sekemu, akawapa masharti na maagizo ya kufuata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ