Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.
Lakini Manase aliwapotosha watu wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema, wakatenda maovu zaidi kuliko mataifa ambayo Yawe aliyaangamiza mbele ya watu wa Israeli.
Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.
Barabara kubwa zimebaki tupu; hakuna anayesafiri kupitia ndani yao. Mapatano yanavunjwa ovyo, washuhuda wanazarauliwa. Hakuna anayejali tena maisha ya wanadamu.
Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.
Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.
Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.
Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.
Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.
Kama mukivunja agano la Yawe, Mungu wenu, ambalo aliwaamuru mulishike, mukienda kuitumikia miungu mingine na kuinama mbele yao; basi, hasira ya Yawe itawaka juu yenu, nanyi mutaangamia mara moja kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.”