Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 24:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Dunia itaharibiwa kabisa na kuangamizwa. Ni Yawe amesema hayo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 24:3
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na hivyo likatimia neno la Yawe alilosema kwa njia ya nabii Yeremia: “Mpaka inchi imetimiza Sabato zake, haitalimwa siku zote itakapokuwa ukiwa mpaka miaka makumi saba itakapotimia.”


Wapigapinde wachache kati ya mashujaa wa watu wa Kedari ndio watakaobaki. Ni Yawe, Mungu wa Israeli, anayesema hivyo.


Lakini siku moja, –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi– ule musumari uliopigiliwa pahali pagumu utaregea kwa uzito. Utakatwa na kuanguka. Yawe amesema.


Sasa Yawe anaiharibu dunia na kuifanya tupu. Atavuruga uso wa dunia na kuwatawanya wakaaji wake.


Kila mutu atapatwa na mambo yaleyale: mutu wa kawaida na kuhani; mutumwa na bwana wake; mujakazi na bibi wake; mwenye kununua na mwenye kuuzisha; mukopeshaji na mukopaji; mwenye kudai na mwenye kudaiwa.


Dunia inakauka na kunyauka; ulimwengu unafazaika na kunyauka; mbingu zinafazaika pamoja na dunia.


Lakini hawa ni watu walioibwa mali yao na kunyanganywa! Wote wamenaswa katika mashimo, wamefungwa katika kifungo. Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa, wamekamatwa mateka na hakuna anayesema: Muwarudishe!


Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Enyi Waisraeli, musikilize kwa uangalifu, musikuwe na kiburi maana Yawe anasema nanyi.


Kwa hiyo, enyi milima ya Waisraeli, musikie neno la Bwana wenu Yawe. Anasema juu ya ninyi milima na vilima, mifereji na mabonde, jangwa tupu na miji ya matongo, na miji iliyokamatwa mateka na kuzarauliwa na mataifa yote yanayowazunguka.


Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo, watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema: Tumeangamia kabisa; amekamata inchi yetu, ameiondoa katika mikono yetu. Mashamba yetu ameyagawanya kwa wale waliotuteka.


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’


“Mambo ya siri ni ya Yawe, Mungu wetu, lakini yale ambayo ameyafunua ni yetu na wazao wetu milele, kusudi tushike maneno yote ya sheria hii.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ