Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.
Yawe anasema hivi: Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake, waovu kwa sababu ya makosa yao. Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno, na kuporomosha mazarau ya watu wakali.
Bwana wetu Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya Gogi. Useme: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Gogi mutawala mukubwa wa mataifa ya Meseki na Tubali.
Yawe anasema hivi: Katika siku ile ya karamu yangu, nitawaazibu wakubwa wa watu hao, vilevile na wana wa mufalme pamoja na wote wanaoiga desturi za kigeni.
Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”
Wafalme wa dunia waliozini nao na kujifurahisha pamoja nao wataulilia na kuufanyia kilio wakati watakapoona moshi wa moto utakaouteketeza ukipanda juu.