Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 24:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia, nyimbo za kumusifu Mungu anayekuwa mwenye haki. Lakini mimi ninasema: Ninakonda, kweli ninakonda. Ole kwangu mimi! Wadanganyifu wanaendelea kuwa wadanganyifu, udanganyifu wao unazidi kuwa mubaya zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 24:16
41 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye akawapa kile walichoomba, lakini akaleta magonjwa makali kati yao.


Ninapowaona waasi hao ninachukizwa sana, kwa sababu hawashiki amri zako.


Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako, na dunia nzima kuwa mali yako.


Mbele hawajatambua, waongolewe kama miiba, michongoma au magugu. Kwa hasira ya Mungu, wapeperushwe mbali, wakikuwa bado wazima.


Unatuliza uvumi wa bahari na wa mawimbi yake, unakomesha fujo za watu.


Inchi imetoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, ametubariki.


Amekumbuka wema na uaminifu wake kwa Waisraeli. Pande zote za dunia zimeuona ushindi wa Mungu wetu.


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi, atawaletea waaskari wao wanene ugonjwa wa kuwakondesha, na utukufu wao utateketezwa kama kwa moto.


Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.


Siku hiyo, utukufu wa Yakobo utaporomoshwa, na unono wake utapotea.


Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.


Umezidisha taifa letu, ee Yawe, umelizidisha taifa letu. Umeipanua mipaka yote ya inchi, kwa hiyo wewe unatukuzwa.


Siku ile Yawe wa majeshi atakuwa taji tukufu, kama kitambaa kizuri kwa watu wake watakaobaki wazima.


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Haujapata kuyasikia wala kuyajua hata kidogo; tangu zamani masikio yako hayakuyasikia. Nilijua kwamba wewe ni mudanganyifu, na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?


Hata wandugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao vilevile wanakudaganya; wanakukaripia waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, ingawa wanakuambia maneno mazuri.


Lakini kama muke asiyekuwa mwaminifu anavyomwacha mume wake, ndivyo ulivyokosa uaminifu kwangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kweli, watu wa Israeli na watu wa Yuda, wamekosa kabisa uaminifu kwangu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Unalia usiku kucha; machozi yanatiririka juu ya mashavu yake. Hakuna hata mumoja kati ya wapenzi wake kwa kuufariji. Rafiki zake wote wameudanganya; wamekuwa waadui zake.


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Lakini mulivunja agano langu kama mulivyofanya katika muji wa Adamu; kule walikosa uaminifu kwangu.


Kama wamoja kati yenu wakibakia katika inchi za waadui zenu watakonda na kuisha kwa sababu ya uovu wao na kwa sababu ya uovu wa wazee wao.


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Wewe ni mutakatifu kabisa, hauwezi kutazama uovu, hauwezi kuvumilia hata kidogo kuona mabaya. Mbona basi unawaona wafanya maovu na kunyamaza, kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao?


Kwa nini unaniachilia kuona mabaya na taabu? Uharibifu na mateso makali vinanizunguka, ugomvi na mabishano yanatokea.


Halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, naye atakusanya watu wake aliowachagua kutoka katika dunia nzima.


Kwa maana Bwana ametuagiza hivi: ‘Nimekuweka kuwa mwangaza wa mataifa, kusudi watu wapate kuokolewa katika dunia yote.’ ”


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ