Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 24:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Muji wa fujo umejaa uharibifu; kila nyumba imefungwa kusudi mutu asiingie.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 24:10
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Muji ule ukaitwa Babeli, kwa sababu kule ndiko Yawe alikovuruga luga ya dunia yote, na tokea kule akawatawanya watu kila pahali katika dunia.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.


Ujumbe wa Mungu juu ya Tiro. Muomboleze, enyi mashua makubwa za kutoka Tarsisi. Kivuko na muji wenu vimeharibiwa. Mutapokea habari hizo mutakaporudia kutoka Kipuro.


Muji ni mabomoko matupu; milango yake imevunjwavunjwa.


Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.


Amewaporomosha waliokaa pande za juu, muji wenye utukufu ameuangusha mpaka chini, ameutupa mpaka katika mavumbi.


Muji ule wenye kuta sasa umekuwa mutupu, umeachwa na kuhamwa kama jangwa, humo ngombe wanakula na kupumzika.


Maana nyumba ya kifalme itaachwa ukiwa, muji huo wa watu wengi utahamwa. Mulima na munara wa ulinzi utakuwa mapango milele, punda wa mwitu watapitapita huko kwa furaha, kondoo watapata malisho yao humo.


Lakini mvua ya mawe itanyesha na kuangusha pori, na muji wake utaangamizwa.


Itakuwa makao ya ndege za jangwa: kozi, bundi na kibombobombo. Yawe atawaletea muvurugano, na timazi la fujo kwa wakubwa wake.


Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani.


Wakaldea waliichoma kwa moto nyumba ya kifalme na nyumba za watu; vilevile walizibomoa kuta za Yerusalema.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa na waaskari walikimbia. Wakatoka inje ya muji wakati wa usiku wakipitia njia ya mulango katikati ya kuta mbili, kwenye bustani ya mufalme, ingawa Wakaldea walikuwa wameuzunguka muji wote. Wakakimbia kuelekea bonde la muto Yordani.


Yule atakayepasua njia atawatangulia, nanyi mutauvunja mulango wa muji na kutoka inje, mutapita na kutoka inje. Mufalme wenu, atawatangulia; Yawe mwenyewe atawatangulia.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Kwa maana siku zitakufikia wakati waadui zako watakapokuzunguka kwa vita, watakapojenga ukuta wa kujikingia pembeni yako, na kukusonga pande zote.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Halafu akalalamika kwa sauti kubwa, akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa ule muji mukubwa Babeli! Sasa umekuwa makao ya mashetani ya kila namna, ya pepo wachafu, na makimbilio ya ndege wote wachafu na wenye kuchukiza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ