Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 24:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa Yawe anaiharibu dunia na kuifanya tupu. Atavuruga uso wa dunia na kuwatawanya wakaaji wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 24:1
45 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitauazibu Yerusalema kama vile nilivyofanya Samaria, na mufalme Ahabu na wazao wake. Nitasafisha Yerusalema kama vile wanavyosafisha sahani na kuigeuza kisha kusafishwa.


Kumbuka sasa lile ulilomwambia mutumishi wako Musa, uliposema: ‘Kama hamutakuwa waaminifu, nitawatawanya kati ya mataifa.


Yawe anawalinda wageni, anawasaidia wajane na wayatima; lakini anaharibu mipango ya waovu.


Nitazitetemesha mbingu nayo inchi itatikisika katika misingi yake kwa sababu ya kasirani ya Yawe wa majeshi, siku ile ya hasira yangu kali.


Wanakuja kutoka inchi za mbali, wanatoka hata miisho ya dunia: Yawe na silaha za hasira yake anakuja kuiangamiza dunia.


Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


Dunia inavunjikavunjika, inapasuka na kutikiswatikiswa.


Inapepesuka kama mulevi, inayumbayumba kama kibanda. Imelemewa na muzigo wa zambi zake nayo itaanguka wala haitasimama tena.


Muji ule wenye kuta sasa umekuwa mutupu, umeachwa na kuhamwa kama jangwa, humo ngombe wanakula na kupumzika.


Ninyi munafanya mambo kinyume kabisa! Mufinyanzi na udongo ni hali moja? Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza hivi: Wewe haukunitengeneza. Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba; Wewe haujui kitu.


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Kila pigo la azabu ya Yawe juu ya Waasuria litaandamana na mudundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe atapigana na Waasuria.


Mujipige kifua kwa huzuni, muomboleze, juu ya mashamba yaliyokuwa mazuri, juu ya mizabibu iliyokuwa ikizaa sana,


Inchi inaomboleza na kunyauka; pori ya Lebanoni imekauka, bonde zuri la Saroni limekuwa jangwa, kule Basani na mulima Karmeli majani yote yamekauka.


Itawaka usiku na muchana bila kuzimika, moshi wake utapanda juu milele. Inchi itakuwa jangwa siku zote, hakuna atakayepitia huko milele.


Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.


Nitaharibu milima na vilima, na majani yote nitayakausha. Mito ya maji nitaigeuza kuwa inchi kavu, na visima vya maji nitavikausha.


Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.


Kama simba anavyotoka kwenye maficho yake, mwangamizaji wa mataifa ameanza kuja, anakuja kutoka pahali pake, kusudi aharibu inchi yenu. Miji yenu itabaki mabomoko matupu, bila kukaliwa na mutu yeyote.


Kisha, Yohana mwana wa Karea akazungumuza na Gedalia kwa siri kule Misipa, akamwambia: Uniruhusu niende nimwue Isimaeli mwana wa Netania, na hakuna mutu yeyote atakayejua. Kwa nini kumwachilia yeye akuue na Wayuda wote waliokusanyika hapa watawanyike na Wayuda waliobaki waangamie?


Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mufikiri na kuwaita wanawake waombolezaji; muwaite wanawake wanaoelewa nyimbo za kilio.


Miji yenye watu itateketezwa, na inchi itakuwa ukiwa. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Weka chungu kitupu juu ya makaa kipate moto sana, shaba yake ipate moto, uchafu wake uyeyushwe na kutu iunguzwe.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakapokufanya wewe Edomu kuwa jangwa, dunia yote itafurahi


Tena, wewe Yerusalema nitakufanya kuwa ukiwa na kitu cha kuchekelewa kati ya mataifa yanayokuzunguka na mbele ya watu wote wanaopita karibu nawe.


Kisha kutimia kwa wakati wa kushambuliwa kwa muji wa Yerusalema, utachoma sehemu moja ya tatu ya nywele zako katikati ya muji. Sehemu ingine moja ya tatu utaikatakata kwa upanga ukiuzunguka muji. Sehemu ya tatu ya mwisho utaipeperusha kwa upepo, nami nitauchomoa upanga wangu na kuwafuatilia nyuma.


Nitanyoosha mukono wangu juu yao, na kuiharibu inchi yao. Tangu huko katika jangwa upande wa kusini mpaka katika muji wa Dibla kwa upande wa kaskazini, nitaifanya inchi yao kuwa matongo kabisa wasipate pahali pa kuishi. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Pahali pote munapoishi, miji yenu itakuwa ukiwa na sehemu zenu zinazoinuka za kutambikia zitabomolewa, mazabahu zenu zitabomolewa na kuwa ukiwa, sanamu zenu za miungu zitavunjwa na kuharibiwa. Pahali penu pa kufukizia ubani patabomolewa na chochote mulichofanya kitatoweka.


Wakati umetimia, ile siku imekaribia. Mununuzi asifurahi wala muchuuzi asiomboleze; kwa sababu kasirani yangu itawaangukia watu wote.


Baragumu imepigwa na kuwafanya wote wakuwe tayari. Lakini hakuna anayekwenda kwa vita, kwa maana kasirani yangu iko juu ya watu wote.


Milima inatetemeka mbele yake, vilima vinayeyuka. Dunia inatetemeka mbele yake, ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Munyanganye feza, munyanganye zahabu! Mali yake haina mwisho! Kuna wingi wa kila kitu cha bei kali!


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Kwa kuwa hawakuwapata, wakamupeleka Yasoni pamoja na wandugu waamini wengine mbele ya wakubwa wa muji. Wakalalamika wakisema: “Watu hawa walifanya fujo fasi zote na sasa wamefika huku.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.


Ningaliwaangamiza kabisa na kuwafanya wasikumbukwe tena na mutu yeyote,


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ