Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 23:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Umefezeheka, ewe Sidona, muji wenye upango kandokando ya bahari! Bahari yenyewe inatangaza: Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa, wala sijazaa; sikulea vijana wanaume, wala kukomalisha wabinti!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 23:4
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kanana alikuwa babu ya Sidona, muzaliwa wake wa kwanza, na Heti,


hata eneo la inchi yao likakuwa toka Sidona kuelekea upande wa kusini, kuendelea Gerari mpaka Gaza, na kuelekea upande wa mashariki liliendelea kwa Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu mpaka Lasa.


wafalme wote wa Tiro na Sidona; wafalme wa inchi zinazokuwa kandokando ya bahari ya Mediteranea;


Kisha, upeleke ujumbe kwa mufalme wa Edomu, mufalme wa Moabu, mufalme wa Amoni, mufalme wa Tiro na mufalme wa Sidona. Uutume kwa mukono wa wajumbe waliokuja Yerusalema kwa kumwona Zedekia mufalme wa Yuda.


Wewe mwanadamu! Ugeukie upande wa Sidona na kutoa unabii juu yake.


Sema hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Sidona, na kuonyesha utukufu wangu kati yako. Nitakapotimiza hukumu zangu juu yako na kukuonyesha utakatifu wangu, halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe.


Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.


Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”


Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ