Kwa hiyo, Daudi akawakusanya Waisraeli wote katika inchi, tokea kwenye kijito cha Sihori kinachokuwa Misri, mpaka kwenye kiingilio cha Hamati kwa kulileta Sanduku la Agano toka Kiriati-Yearimu.
Halafu, watu wote watakaoomba kwa jina la Yawe wataokolewa. Katika mulima Sayuni na Yerusalema, kutakuwa watu watakaoponyoka, kama vile Yawe alivyosema: wale aliowachagua watabaki wazima.
Inchi munayokwenda kurizi si kama inchi ya Misri mulikotoka, ambako mulipanda ngano nanyi mulipaswa kuleta maji kutoka kwenye mito kwa kuimwangilia kama vile mulivyofanya kwa mashamba ya mboga.
ni kusema eneo linalojulikana kama la Wakanana, kuanzia kwenye kijito cha Sihori kwa mupaka wa Misri mpaka kwenye eneo la Ekuroni kule kaskazini. Maeneo yote ya watawala watano wa Wafilistini: Gaza, Asidodi, Asikeloni, Gati na Ekuroni pamoja na eneo la Awini,