Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 23:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha miaka hiyo makumi saba, Yawe atauazibu muji wa Tiro, nao utarudia kufanya uzinzi kwa kujiuzisha kwa mataifa yote ya dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 23:17
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo muji wa Tiro utasahauliwa kwa muda wa miaka makumi saba, muda wa maisha ya mufalme. Kisha miaka hiyo makumi saba, muji wa Tiro utapatwa na kile watu wanachoimba juu ya kahaba:


Kamata kinubi chako uzungukezunguke ndani ya muji, ewe kahaba uliyesahauliwa! Imba nyimbo tamutamu. Imba nyimbo nyinginyingi, kusudi upate kukumbukwa tena.


Inchi hii yote itakuwa katika mabomoko matupu na ukiwa, na mataifa jirani yatamutumikia mufalme wa Babeli kwa muda wa miaka makumi saba.


Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.


Kwa mwanzo wa kila barabara ulijijengea nafasi inayoinuka, ukautumia uzuri wako kwa kufanya uzinzi ukijitoa kwa kila mupita njia na kuongeza uzinzi wako.


Tena ulifanya uzinzi na jirani zako Wamisri waliojaa tamaa, ukaongeza uzinzi wako na kuichochea hasira yangu.


Umejijengea nafasi yako yenye kuinuka kwa mwanzo wa kila barabara na kujijengea pahali pa kutambikia katika kila kiwanja. Tena wewe haukukuwa kama kahaba maana ulikataa kulipwa.


Nimekunja ngumi yangu juu yako kwa sababu ya hiyo faida uliyopata kwa njia isiyokuwa ya haki na kwa mauaji yaliyofanyika kwako.


Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa, kila kitu kilichochumwa kitateketezwa kwa moto. Nitaharibu sanamu za miungu yake yote. Zililundikwa kutokana na mushahara wa ukahaba, nazo zitatumiwa tena kuwa mushahara wa ukahaba.


Waamuzi wanahukumu kwa kupewa kutuliro, makuhani wake wanafundisha kwa kupata malipo, manabii wanatabiri kwa kupata feza. Hata hivyo wanajidai kumutegemea Yawe, wakisema: Yawe, si yupo pamoja nasi? Hatutapatwa na hasara yoyote!


Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba. Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi, uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako, na watu wa mataifa kwa uchawi wako.


Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.


Simoni anatoka kutuelezea namna Mungu alivyowashugulikia watu wa mataifa mengine pale mbele kusudi ajichagulie wamoja kati yao kuwa watu wake wa pekee.


“Mwisraeli yeyote, mwanaume au mwanamuke, hatakuwa hata kidogo kahaba wa kidini.


Hapaswi kuwa mulevi wala mupiganaji, lakini akuwe mupole mwenye kupenda amani, wala asikuwe mutu wa kupenda feza.


Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ