Hapo muji wa Tiro utasahauliwa kwa muda wa miaka makumi saba, muda wa maisha ya mufalme. Kisha miaka hiyo makumi saba, muji wa Tiro utapatwa na kile watu wanachoimba juu ya kahaba:
Wapenzi wako wote wamekusahau; hawajali kitu chochote juu yako. Nimekupiga sawa vile ungekuwa adui yangu. Umeazibiwa bila huruma, kwa sababu kosa lako ni kubwa, zambi zako ni nyingi sana.
Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba. Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi, uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako, na watu wa mataifa kwa uchawi wako.