Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 23:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 (Ni Wakaldea, wala si Waasuria, waliowaacha nyama wa pori waushambulie muji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia muji huo minara ya kuushambulia, wakabomoa nyumba zake na kuufanya mabomoko.)

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 23:13
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Huyo Harani alikufa wakati baba yake Tera alikuwa anaishi kule Uri, muji wake wa kuzaliwa.


Tera akatwaa Abramu mwana wake, Loti mujukuu wake aliyekuwa mwana wa Harani, na Sarai muke wa Abramu, wakaondoka wote pamoja toka Uri, muji wa Wakaldea, na kwenda katika inchi ya Kanana. Lakini walipofika Harani, wakakaa pale.


Muji ule ukaitwa Babeli, kwa sababu kule ndiko Yawe alikovuruga luga ya dunia yote, na tokea kule akawatawanya watu kila pahali katika dunia.


Jina la muto wa tatu ni Tigre, nao unatiririkia upande wa mashariki wa inchi ya Asuria. Jina la muto wa ine ni Furati.


Kisha mufalme wa Asuria akapeleka watu kutoka Babeli, Kuta, Awa, Hamati na Sefarwaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria kwa pahali pa watu wa Israeli waliopelekwa katika uhamisho. Wakaitwaa miji hiyo na kukaa mule.


Wakati ule, mufalme Berodaki-Baladana mwana wa Baladani mufalme wa Babeli alisikia kwamba Hezekia alikuwa amegonjwa na sasa amepona, alimutumia ujumbe pamoja na zawadi.


Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.


Yule naye alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Wakaldea walijipanga makundi matatu, wakashambulia ngamia, wakawatwaa, na wakaua watumishi wako kwa upanga! Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Waadui zake wanaokaa katika jangwa wanyenyekee mbele yake, wapinzani wake walambule vumbi.


Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!


Lakini Asuria hakuwazia hivyo, yeye alikuwa na nia ingine; alikusudia kuharibu kabisa, kuangamiza mataifa mengi sana.


Babeli ni utukufu wa falme zote na sifa na majivuno ya Wakaldea utakuwa kama Sodoma na Gomora, wakati Mungu alipoiangamiza.


Pahali pake ni nyama wakali wa pori ndio watakuwa ndani yake, bundi watajaa katika nyumba zake. Mbuni wataishi humo, pepo watachezea huko.


Yote yataachiwa ndege wa milima na nyama wengine wa pori. Ndege wakali watakaa humo wakati wa jua, na nyama wa pori watafanya makao humo wakati wa baridi.


Yawe, Mukombozi wenu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Kwa ajili yenu nitatuma waaskari kwenda Babeli. Nitavunja vifungio vya milango ya muji wake, na kelele za wale Wakaldea zitageuka maombolezo.


Nitawachochea Wababeli na Wakaldea wote, watu toka Pekodi, Soa na Koa, pamoja na Waasuria wote. Nitawachochea vijana wote wa kuvutia, maliwali, waamuzi, majemadari na waaskari wote wakiwa wapanda-farasi.


Wewe mwanadamu! Nebukadneza, mufalme wa Babeli, aliwalazimisha waaskari wake kufanya kazi ngumu ya kuishambulia Tiro. Vichwa vyote vya waaskari wake vilipata upaa na mabega yote yalichubuka. Lakini yeye, wala waaskari wake, hawakupata chochote kutokana na kazi hiyo aliyoifanya juu ya Tiro.


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Maana ninawachochea Wakaldea, taifa lile kali na lenye nguvu, taifa linalopita katika inchi yote, kwa kunyanganya makao ya watu wengine.


Basi Abrahamu akatoka katika inchi ya Wababeli akaenda kukaa Harani. Kisha kufa kwa baba yake, Mungu akamuhamisha tena, akakuja kukaa katika inchi hii munayoishi ndani yake sasa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ