Shuka, uikae katika mavumbi, ewe bikira, binti wa Babeli! Ikaa chini pasipo kiti cha kifalme, ewe binti wa Wakaldea! Tokea sasa hautaitwa tena murembo wala mwenye kupendeza.
Yawe aliwakataa waaskari walionilinda, alitangaza wakati kamili wa kuniazibu kuwaponda vijana wangu wanaume. Aliwaponda kama katika kikamulio, watu wangu wa Yuda.
Watu wa Yuda wamekwenda katika uhamisho, wakijaa mateso na kuwa katika utumwa mukali. Wanakaa kati ya watu wa mataifa, wala hawapati nafasi ya kupumzikia. Waliowafuatilia wamewakamata wakiwa katika taabu.
Watu waliwapigia kelele wakisema: Mutoke, enyi munaokuwa wachafu! Mutoke! Mutoke! Musiguse kitu chochote. Hivyo wakakuwa wakimbizi na kutangatanga; watu wa mataifa walisema: Hawa hawatakaribishwa kukaa kwetu!
Walitwaa miti ya mialo toka Basani wakakuchongea makasia; walikutengenezea mbao za kuikalia kwa miti ya misunobari ya kisanga cha Kipuro, na kuipamba kwa pembe ya tembo.
Mashua kutoka Kitimu zitamushambulia, naye atashikwa na hofu. Kisha atarudi nyuma akiwa amejaa hasira na kuvunja agano takatifu. Halafu atafuata shauri la wale walioasi agano takatifu.
Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.
Sauti ya wapiga vinubi na ya wapiga vinanda, ya wapiga filimbi na ya baragumu, haitasikilika ndani yako tena. Fundi wa kazi yoyote hataonekana ndani yako tena hata kidogo wala kelele la jiwe la kusagia halitasikilika.