Isaya 23:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Ujumbe wa Mungu juu ya Tiro. Muomboleze, enyi mashua makubwa za kutoka Tarsisi. Kivuko na muji wenu vimeharibiwa. Mutapokea habari hizo mutakaporudia kutoka Kipuro.
Kwa sababu mufalme Solomono alikuwa na mashua kubwa za Tarsisi zilizokuwa zikisafiri pamoja na mashua za Hiramu, kisha kila miaka mitatu mashua hizo za Tarsisi zilimuletea mufalme zahabu, feza, pembe, kima, na tausi.
Solomono alitawala falme zote kuanzia kwa muto Furati mpaka katika inchi ya Wafilistini, na kuendelea hata kwa mupaka na Misri. Mataifa yote yalimutumikia na kulipa kodi kwake wakati wote wa maisha yake.
Solomono alikuwa na mashua zilizosafiri mpaka Tarsisi na watumishi wa Hiramu, na kisha kila miaka mitatu, mashua zile zilirudi zikimuletea zahabu, feza, pembe, kima na ndege wanaoitwa tausi.
Ni mashua zinazotoka katika inchi za mbali, zikitanguliwa na mashua za Tarsisi. Zinawaleta watoto wako, pamoja na feza na zahabu yao, kwa sifa ya Yawe, Mungu wako, kwa sifa ya Mungu, Mutukufu wa Israeli, maana amewafanya mupate utukufu.
Yawe, Mungu wa Israeli, akaniambia hivi: Twaa toka katika mukono wangu kikombe hiki cha divai kinachojaa kasirani yangu uyakunyweshe mataifa yote ninayokutuma kwao.
Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilistini wote, kukomesha musaada uliobakia kutoka Tiro na Sidona. Maana Yawe anawaangamiza Wafilistini, watu waliobaki wa kisanga cha Kafutori.
Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!
Walitwaa miti ya mialo toka Basani wakakuchongea makasia; walikutengenezea mbao za kuikalia kwa miti ya misunobari ya kisanga cha Kipuro, na kuipamba kwa pembe ya tembo.
Mashua kutoka Kitimu zitamushambulia, naye atashikwa na hofu. Kisha atarudi nyuma akiwa amejaa hasira na kuvunja agano takatifu. Halafu atafuata shauri la wale walioasi agano takatifu.
Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.
Yesu akaendelea kusema: “Ole kwako muji Korazini! Ole kwako muji Betesaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika ndani yenu ingefanyika katika muji wa Tiro na wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuonyesha masikitiko yao kwa kuvaa magunia na kujipakaa majivu, na kugeuka toka zambi zao.
Hapo, mupaka uligeuka kuelekea Rama na kufikia kwenye muji wa Tiro uliokuwa na kuta. Kisha ukageuka kuelekea Hosa na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. Miji mingine iliyokuwa katika eneo lile ni Maharabu, Akizibu,