Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.
Nitavivunjavunja vifungio vya milango ya muji wa Damasiki, na kuwaondoa wakaaji wa bonde la Aweni, pamoja na mutawala wa Beti-Edeni. Waaramu wanapelekwa katika uhamisho kule Kiri. –Ni Yawe anayesema hivyo.
Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.