Kwa hiyo, si ninyi mulionileta huku, lakini ni Mungu. Ndiye aliyenifanya kama baba kwa mufalme wa Misri, musimamizi wa nyumba yake yote na mutawala wa inchi yote ya Misri.
Mordekayi alipotoka katika nyumba kwa mufalme, akiwa amevaa nguo ya kifalme ya rangi ya mayungiyungi na nyeupe, koti la kitani safi la rangi nyekundu, na taji kubwa ya zahabu, muji wa Susani ukajaa shangwe na vigelegele.