Isaya 22:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200215 Bwana wetu Yawe wa majeshi aliniambia niende kwa Sebuna, musimamizi wa jamaa ya kifalme, nimwambie hivi: အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Hawa ni wasimamizi wa mali ya mufalme Daudi: Azimaweti mwana wa Adieli alisimamia hazina za mufalme Daudi. Yonatani mwana wa Usia alisimamia hazina zilizokuwa katika inchi, miji, vijiji na katika minara. Ezeri mwana wa Kalebu alisimamia walimaji. Simei wa muji wa Ramati alisimamia kazi ya mashamba ya mizabibu. Zabudi wa muji wa Sifi alisimamia mazao ya mashamba ya mizabibu. Bali-Hanani wa muji wa Gederi alisimamia mizabibu na mikuyu ya inchi ya Shefela. Yoasi alisimamia gala za mafuta. Sitirayi wa muji wa Saroni alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa kule Sarani. Safati wa muji wa Adilai alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa katika mabonde. Obili Mwisimaeli alisimamia ngamia. Yedeya, Mumeronoti alisimamia punda dike. Yasisi, Muhagri, alisimamia makundi ya kondoo.