Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 22:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Bwana wetu Yawe wa majeshi aliniambia niende kwa Sebuna, musimamizi wa jamaa ya kifalme, nimwambie hivi:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 22:15
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo mukubwa wa nyumba ya mufalme na musimamizi wa muji, wakishirikiana na viongozi wengine na walinzi, wakamupelekea Yehu ujumbe huu: “Sisi ni watumwa wako, na tuko tayari kufanya lolote unalosema. Lakini hatutamuweka mutu yeyote kuwa mufalme. Fanya unavyotaka.”


Walipomwita mufalme Hezekia walipokelewa na Eliakimu mwana wa Hilkia ambaye alikuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa mwandishi wa mufalme, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wa habari.


Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia, Sebuna na Yoa wakamujibu yule jemadari: “Tafazali, useme nasi kwa luga ya Kiaramea maana tunaielewa. Usiseme nasi kwa luga ya Kiebrania. Watu wanaokuwa juu ya ukuta wanasikia.”


Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi, wakamwendea Hezekia wakiwa na nguo zenye kupasuliwa, wakamwelezea maneno ya yule jemadari.


Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna mwandishi, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.


Hawa ni wasimamizi wa mali ya mufalme Daudi: Azimaweti mwana wa Adieli alisimamia hazina za mufalme Daudi. Yonatani mwana wa Usia alisimamia hazina zilizokuwa katika inchi, miji, vijiji na katika minara. Ezeri mwana wa Kalebu alisimamia walimaji. Simei wa muji wa Ramati alisimamia kazi ya mashamba ya mizabibu. Zabudi wa muji wa Sifi alisimamia mazao ya mashamba ya mizabibu. Bali-Hanani wa muji wa Gederi alisimamia mizabibu na mikuyu ya inchi ya Shefela. Yoasi alisimamia gala za mafuta. Sitirayi wa muji wa Saroni alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa kule Sarani. Safati wa muji wa Adilai alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa katika mabonde. Obili Mwisimaeli alisimamia ngamia. Yedeya, Mumeronoti alisimamia punda dike. Yasisi, Muhagri, alisimamia makundi ya kondoo.


Kisha Eliakimu, Sebuna na Yoa wakamujibu yule jemadari: “Tafazali useme nasi kwa luga ya Kiaramea maana tunaielewa. Usiseme nasi kwa luga ya Kiebrania. Watu wanaokuwa juu ya ukuta wanasikia.”


Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi, wakamwendea Hezekia na nguo zenye kupasuliwa, wakamwelezea maneno ya yule jemadari.


Nao walikutana na Eliakimu mwana wa Hilkia, aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, aliyekuwa katibu, pamoja na mwandishi Yoa mwana wa Asafu.


Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.


Basi Filipo akajitayarisha na kwenda. Alipokuwa katika njia, mara moja akakutana na towashi mumoja Mwetiopia. Mutu huyu alikuwa mukubwa, alishugulika na kazi ya usimamizi wa mali zote za malkia Kandake wa Etiopia. Yeye alikuwa amekwenda Yerusalema kwa kumwabudu Mungu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ