Nabii Yeremia vilevile akatunga shairi la maombolezo kwa ajili ya kifo chake; nao waimbaji wote, wanaume na wanawake, wanamutaja Yosia katika maombolezo yao, mpaka leo. Wakakusudia kuwa wanafanya maombolezo haya katika Israeli; angalia nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.
Watu wa Diboni wamepanda katika hekalu pahali pa juu kwa kuomboleza, watu wa Moabu wanalia kwa ajili ya Nebo na Medeba; vichwa vyote vimenyolewa upaa, ndevu zao zote zimekatwa kabisa.
Lakini waovu hata wakipewa rehema, hawawezi kujifunza kutenda haki. Hata katika inchi ya usawa, wao bado wanatenda maovu, wala hawajali ukubwa wako wewe Yawe.
Kwa pahali pa harufu ya marasi watatoa uvundo; kwa pahali pa mikaba mizuri watatumia kamba; kwa pahali pa nywele nzuri watakuwa na upaa; kwa pahali pa nguo nzuri watavaa magunia; uzuri wao wote utageuka kuwa haya.
Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.
Ninyi munaniuliza: Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni? Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali? Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula, munatafuta tu furaha yenu wenyewe na kuwagandamiza watumishi wenu!
Wote, wakubwa kama vile wadogo, watakufa katika inchi hii; nao hawatazikwa, wala hakuna atakayeomboleza juu yao. Hakuna atakayejikatakata wala kunyolewa upaa kwa ajili ya kifo chao.
Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.
Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.
Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?
Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.
Habari hizi zikamufikia mufalme wa Ninawe, naye akaondoka juu ya kiti chake cha kifalme, akavua nguo yake ya kifalme, akavaa gunia na kuikaa katika majivu.
Enyi watu wa Yuda, munyoe vichwa vyenu kwa kuwaomboleza watoto wenu wapenzi; mupanue upaa wenu ukuwe mupana kama wa tai, maana watoto wenu watawaacha kwenda katika uhamisho.