Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 22:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Katikati ya kuta hizo mulijijengea birika la kulinda maji yanapotiririka kutoka birika la zamani. Lakini hamukumutafuta Mungu aliyepanga mambo haya yote; hamukumujali yeye aliyepanga hayo yote tangu zamani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 22:11
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Matendo mengine ya Hezekia, ushujaa wake na maelezo juu ya jinsi alivyojenga kisima na kuchimba mufereji wa kuleta maji katika muji, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.


Lakini kisha nilichagua muji wa Yerusalema ukuwe muji ambamo nitaabudiwa, na nilimuchagua Daudi awatawale watu wangu Waisraeli.’


Sehemu inayofuata mpaka kwenye makaburi ya Daudi, kisima na majengo ya waaskari ikajengwa upya na Nehemia mwana wa Aibuki, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Beti-Suri.


Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mutakatifu wa Israeli.


Mulizikagua nyumba za Yerusalema, mukazibomoa kwa kupata mawe ya kukaza kuta za muji.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Haujasikia, ewe Saniharibu, kwamba mimi Yawe nilipanga jambo hili tangu zamani? Ninachotimiza sasa nilikipanga zamani. Nilikuweka uifanye miji yenye kuzungukwa na kuta kuwa lundo la mabomoko.


Yawe akamwambia Isaya: Uende pamoja na mwana wako anayeitwa Watakaobaki-Watarudi, kukutana na mufalme Ahazi. Utamukuta katika barabara pahali wafuaji wa nguo wanapofanyia kazi, mwisho wa mufereji unaoleta maji kutoka kwenye birika la juu.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ