Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.
Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.
Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.
Sasa mimi nitapigana nanyi: ninyi munaoishi katika bonde, munaokaa kwenye mawe katika uwanja, ninyi munaosema: Nani atasubutu kutushambulia? Nani anayeweza kuingia katika makao yetu?
Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.
Juu ya nyumba za Moabu na katika viwanja vyao hakuna kinachosikilika lakini maombolezo tu. Mimi nimemuvunja Moabu kama chombo kisichotakiwa na mutu. –Ni ujumbe wa Yawe.
Nitawaangamiza wote wanaoinama juu ya dari, wakiabudu jeshi la mbinguni. Nitawaangamiza wale wanaoniabudu na kuapa kwa jina langu, tena wanaapa vilevile kwa jina la mungu Milkomu.
Sasa, Saulo alikuwa anatoka kwenye shamba akiwa na ngombe dume wake, akauliza: “Watu wana nini? Kwa nini wanalia?” Wakamwambia habari wajumbe waliyoleta kutoka Yabesi.
Wakati huo, kijana Samweli alipokuwa anamutumikia Yawe chini ya uangalizi wa Eli, ujumbe kutoka kwa Yawe ulikuwa mara haba tu; hata na maono kutoka kwake yalipatikana mara chache.