Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 22:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ujumbe wa Mungu juu ya Bonde la Maono. Kuna nini, ee Yerusalema? Mbona watu wote mumepanda juu ya nyumba?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 22:1
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.


Mufalme akamwambia: “Una shida gani?” Yule mwanamuke akajibu: “Ninasikitika, mimi ni mujane, mume wangu amekufa.


Shida yako ni nini?” Akamujibu: “Juzi mwanamuke huyu alinishauria tumukule mwana wangu na kesho yake tutamukula wake.


Ee bahari, nini iliyokufikia hata ukakimbia? Nawe Yordani, kwa nini uliacha kutiririka?


Kama vile milima inavyozunguka Yerusalema, ndivyo Yawe anavyozunguka watu wake, tangu sasa na hata milele.


Pasipo maono ya kinabii, watu wanashindwa kujizuiza. Heri mutu yule anayeshika sheria.


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


Wanapita katika njia wakivaa magunia. Kwenye paa za nyumba na viwanja vya muji watu wanalia na kukauka kwa machozi.


Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.


Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.


Sasa mimi nitapigana nanyi: ninyi munaoishi katika bonde, munaokaa kwenye mawe katika uwanja, ninyi munaosema: Nani atasubutu kutushambulia? Nani anayeweza kuingia katika makao yetu?


Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.


kwa sababu ya uovu wote watu wa Israeli na Wayuda waliotenda, pamoja na wafalme na wakubwa wao, makuhani na manabii wao, na wakaaji wa Yerusalema.


Juu ya nyumba za Moabu na katika viwanja vyao hakuna kinachosikilika lakini maombolezo tu. Mimi nimemuvunja Moabu kama chombo kisichotakiwa na mutu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono, kutakuwa giza kwenu bila ufunuo. Jua litatua juu yenu, na muchana utakuwa giza kwenu.


Nitawaangamiza wote wanaoinama juu ya dari, wakiabudu jeshi la mbinguni. Nitawaangamiza wale wanaoniabudu na kuapa kwa jina langu, tena wanaapa vilevile kwa jina la mungu Milkomu.


Neno ninalowaambia katika giza, muliseme muchana kati. Vilevile neno munalosikia kwa siri, mulitangaze mukisimama juu ya paa ya nyumba.


Kuna faida kubwa sana kila upande. Kwanza, Mungu alifunua Neno lake kwa Wayuda kusudi walishike.


“Unapojenga nyumba, jenga ukuta pembeni ya paa, kusudi usihukumiwe kama mutu akianguka kutoka huko, na kufa.


Kisha wakawapigia kelele, nao watu wa kabila la Dani wakageuka, wakamwuliza Mika: “Una shida gani hata umetufuatilia pamoja na kundi hili lote?”


Sasa, Saulo alikuwa anatoka kwenye shamba akiwa na ngombe dume wake, akauliza: “Watu wana nini? Kwa nini wanalia?” Wakamwambia habari wajumbe waliyoleta kutoka Yabesi.


Wakati huo, kijana Samweli alipokuwa anamutumikia Yawe chini ya uangalizi wa Eli, ujumbe kutoka kwa Yawe ulikuwa mara haba tu; hata na maono kutoka kwake yalipatikana mara chache.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ