6 Bwana aliniambia: Kwenda uweke mulinzi; umwambie atangaze atakachoona.
Huyo mulinzi akasema kwa sauti, akamwambia mufalme. Mufalme akasema: “Kama yuko peke yake, ni kusema ana habari.” Yule mutu akazidi kukaribia.
Walinzi wa muji waliniona walipokuwa wanazunguka katika muji. Basi nikawauliza: Mumemwona mupenzi wangu wa moyo?
Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;
Wewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mulinzi wa Waisraeli. Utakuwa ukisikiliza maneno ninayokuambia na kwenda kuwatolea maonyo yangu.