Hamani akaendelea kujitapa: “Vilevile malkia Esteri hakumwalika mutu mwingine yeyote pamoja na mufalme isipokuwa mimi tu. Hata kesho tena, ametualika mimi na mufalme.
Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.
Wakiwa na hamu kubwa nitawatayarishia karamu: nitawalewesha mpaka wapepesuke; nao watalala usingizi wa siku zote na hawataamuka tena. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!
Saa ileile, vidole vya mukono wa mwanadamu vikatokea na kuandika kwenye lipu ya ukuta wa nyumba ya kifalme uliopakaliwa chokaa pahali palipoangaziwa vizuri, mbele ya kinara cha taa. Mufalme aliuona mukono ule ukiandika.